Monday, February 9, 2009

Korogwe Chuo cha Ualimu!!

Hapa ni kwenye lango kuu kuingia chuoni.

Ni chuo kilichopo mkoani Tanga katika wilaya ya Korogwe. Ni moja kati ya vyuo vikongwe kabisa hapa nchini ambapo walimu wetu wengi wamepita na kujizolea "teaching Pedagogy". Ni mahala pazuri pa kutembelea!

Karibuni kwa maoni

9 comments:

Simon Kitururu said...

Nawasiwasi na uraia wa hizo sanamu!:-)Huko naogopa kuja nasikia wanawake wa Kitanga wanaweza kubakiza mtu kwa mahaba huko!:-)

Eee bwana eeh!Napita tu kukusabahi hapa kijiweni Mkuu!

Siku Njema!

Anonymous said...

Safi sana mkuu nimefurahi kuona picha ya chuo nina Bro wangu anaishi hapo korogwe, Natamani kama unapicha zaidi za korogwe unipatie, Na Simon unanifurahisha na joke yako.

Anonymous said...

Asante ndugu Mtanzania tuzidi kuwasiliana we r all TZ.

Anonymous said...

nimefurahi sana kuona chuo cha korogwe kwakua na mimi naishi korogwe ila kwa sasa niko nje ya hapo.natoa ushauri kuwa mabweni yaboreshwe kwakua yako kama viota vya ndege.all the best kazi nzuri.

Anonymous said...

MSELEM
chuo kizuri sana ila mabweni.mpaka yadondoke?

Unknown said...

Nimesoma hapo miaka mingi iliyopita........darasa langu halikuishia kutoa waalimu tu.....wako wataalamu wa lugha.....wanasheria........pastors.....nk na ndipo tulipokutana na Marehemu Munga Tehenan........!

Anonymous said...

Nasoma hapa na ni mara yangu ya kwanza kutembelea blog hii. chuo cha ualimu korogwe ni moja kati ya vyuo vikubwa na maarufu sana, lakini swala la mbiku ni moja kati ya vitu vinavyo wainua sana wana korogwe ttc, na ni moja ya vitu vinavyo wafanya wafurahie maisha kila inapokuwepo, ingawa haikuandikwa kwenye joining instruction form. lakini pia ni moja kati ya vitu vinavyo shusha taaluma ya KTC, embu cheka kidogo 'Eti mtu anaripoti leo, keshokutwa mbiku ina anza halafu anajikuta haja chaguliwa, anasepa kwao, then akirudi kuna kusoma kimagumashi, then likizo, mara BTP> akirudi anakuja ku uza sura darasani na kuchekacheka bwenini, labda kikubwa atakaccho kifanya ni kulala gest baadhi ya siku. baadhi ya wakufunzi nao ni wachakachuaji kinoma 2nawajua na 2na wa kickback wengine wa umeme, wengine wanajipatia kutoka kwa wanachuo. hyo ndio life style ya korogwe../ miaka miwili ya masomo sawa na miezi mitano.. Chocha maggesa .........anapendw madarasani kuliko wakufunzi wote KTC, jiulize je! kwa7bu anafundisha vizuri sana au kwa7bu ana porojo nyingi akiwa class?? huo ni mtazamo wangu.... my real comment ni kwamba,.. MWIGA ni father wetu na yuko peace sana , ila sipendi tabia ya watu fulani kukimbia kimbia kila wamuonapo,... that is Uoga wa kijinga , mwiga is like every body...

Anonymous said...

Ni chuo kikongwe kwelili, panaonekana pamechakaa, sasa walimu wakitoka hapo wataweza kweli kuweka mazingira ya shule zao katika ukijani na usafi. Panaonekana kama ni Dodoma mvua unanyesha maramoja kwa mwaka, ila Tanga ni nyingi, tabia ya kutojali mazingira ni urithi wetu.

gamoyo said...

VP,Ada Ni shiling ngapi kwa mwaka