Thursday, May 10, 2007

Kama ni urafiki mhh! "hii too much".




Kwa jamii yetu mnyama mbwa anafugwa kwa madhumuni ya kusaidia ulinzi. Ila katika jamii nyingine mnyama huyu ni rafiki mkubwa wa binadamu na anapewa heshima zote za rafiki wa kweli. Kudhihirisha hilo ni kosa kubwa kwa wenzetu hawa kumtaja mnyama huyu kwa kutumia pronoun "it". Huwakilishwa na pronoun sawia kabisa na binadamu. Mathalani mbwa dume ni "he" na mbwa jike ni "she". Huo ni mfano mmoja tu wa heshima apewayo mnyama mbwa. Naamini ipo mingi.

Saturday, May 5, 2007

Ujumbe!

Serikali ya Tanzania imedhamiria kuvitangaza vivutio vilivyopo nchini. Hapa ni siku ujumbe wa Tanzania ulipokitembelea chuo kikuu cha New York kwa ajili hiyo. Timu iliongozwa na Mh. Jumanne Maghembe (Waziri wa maliasili na utalii-wa tatu toka shoto). Pia alikuwepo balozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Mh. Mahiga-wa nne toka kulia.

Wednesday, May 2, 2007

Hivi kumbe KIMWI chamtoto kwa MALARIA!


Tarehe 25/4 ilikuwa siku ya malaria. Kama ilivyo kwa malaria kuna siku ya UKIMWI pia. Inasikitisha kwamba nguvu nyingi zinatumika katika kupambana na UKIMWI huku malaria ikishika kasi katika kusababisha vifo vingi kuliko UKIMWI. Kwa ujumla inasikitisha na kusononesha kusikia kwamba MALARIA bado ni namba one killer desease hapa Tanzania. Sanjari na hilo karibu zaidi ya 80% ya wagonjwa wanasumbuliwa na malaria huku wengi wao wakiwa watoto na akina mama wajawazito. Nini kifanyike maana malaria inasababisha vifo vingi?