
Pengine kusimama kwa uwanja mpya wa michezo ni miongoni mwa mambo yatayotufanya watanzania tusiisahau serikali ya awamu ya tatu. Tayari maandalizi ya ufunguzi wa kiwanja hicho cha michezo yanazidi kushika kasi. Real Madrid moja ya timu kubwa tena tajiri pengine kuliko vilabu vingine duniani imekubali kushiriki sherehe za uzinduzi wa uwanja huu kwa kutoa masharti magumu ikiwa ni pamoja na kupatiwa tiketi za ndege kwa ajili ya msafara wa watu 80 (round trip) kutoka Dar hadi Madrid-Hispania. Japo mwaliko huo ulitolewa na serikali na pia gharama zote zitalipwa na serikali bado hakukuwa na ulazima sana wa kujiingiza katika gharama kubwa kwa ajili ya timu moja (Real Madrid). Ingependeza kama zingealikwa timu za taifa kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika kama vile Togo, Nigeria, Afrika ya Kusini, Misri n.k. Hii ingetosha kabisa kuchagiza sherehe za ufunguzi wa uwanja mpya. Lakini pia ingekuwa ni manufaa makubwa katika kuijenga timu yetu ya taifa kimazoezi kwa kucheza na timu za taifa kutoka mataifa mbalimbali. Wewe unasemaje?