Friday, March 2, 2007

Chuo Kikuu cha New York kuwa na tawi Tanzania, chatengewa ekari 500!

Waziri wa Mali asili na utalii Prof. J4 Maghembe akiteta jambo na wadau wa Chuo kikuu cha New York ikiwa ni jitihada za serikali ya awamu ya nne kuitangaza Tanzania na vivutio mbalimbali vilivyopo nchini. Wadau wa Chuo kikuu cha New York wameonyesha dhamira ya kufungua tawi la chuo hicho nchini Tanzania. Serikali imekipatia chuo hicho ekari 500 kwa ajili ya kufungua tawi hilo ambalo litaitwa NYU in Tanzania. Akiwa chuoni hapo Waziri wa mali asili na utalii aliwahakikishia uwepo wa eneo hilo. Hiyo ilikuwa tarehe 22/2/ 07. Chuo kikuu cha New York tayari kina matawi nchini Brazil, Canada,Uingereza na Ghana. Huenda Tanzania ikaingia kwenye hiyo orodha.

6 comments:

Anonymous said...

Je wangapi (wazawa) wataweza kulipa ada za chuo hicho?. Hilo tu.

Anonymous said...

Ni kweli fido, wangapi wataweza? Kule Misri kuna American University in Cairo, ukiona vijana wanaosoma pale, basi ujue baba au wazazi wao ni tycoons wa namna fulani. Mtu wa kawaida kwake Cairo university!!! na vinginevyo.

Hapa vijana wanalia na asilimia 40 ya tuhela tudogo, je hiyo asilimia 100 ya mahela kibao!!???

Wazo zuri lakini. Wacha walete tu hicho chuo. Tutalima mchicha na kuwasomesha watoto wetu. Yawezekana.

Anonymous said...

Labda NYU watatoa scolarship! You never know.

Maisha said...

na mashuga mami na mashuga dadi watatulipia walalhoi....heh heh.

mzee wa mshitu said...

Habari hii na mimi niliipata kaka nilipokuwa huko mwanzoni mwa mwaka huu. Ni kweli kabisa nadhani itatusaidia saana walalahoi tupate elimu ya kizungu nyumbani. Si unakumbuka kile chuo cha kitapeli cha Waldolf kililamba pesa na kutokomea.

MTANZANIA. said...

Charahani!
Hawa jamaa wa NYU inaonekana wako makini. Tusuburi, tutayaona. Tusiombe yatokee yale ya Waldolf.