Thursday, May 10, 2007

Kama ni urafiki mhh! "hii too much".




Kwa jamii yetu mnyama mbwa anafugwa kwa madhumuni ya kusaidia ulinzi. Ila katika jamii nyingine mnyama huyu ni rafiki mkubwa wa binadamu na anapewa heshima zote za rafiki wa kweli. Kudhihirisha hilo ni kosa kubwa kwa wenzetu hawa kumtaja mnyama huyu kwa kutumia pronoun "it". Huwakilishwa na pronoun sawia kabisa na binadamu. Mathalani mbwa dume ni "he" na mbwa jike ni "she". Huo ni mfano mmoja tu wa heshima apewayo mnyama mbwa. Naamini ipo mingi.

10 comments:

Simon Kitururu said...

Hawa jamaa na mapenziyao ya mbwa ni kiboko.Unaweza kukuta mbwa anamatumizi makubwa kuliko binadamu kwenye nyumba zao.Na wafanyabiashara walivyo wajanja ,basi utakuta hawa wanasehemu zao mpaka za masaji

Mija Shija Sayi said...

Ndiyo mambo ya tamaduni hayo. Ok, Mtanzania hivi ulishawahi kupitia hapa?

http://www.blogutanzania.blogspot.com/

Kama bado pitia na uchukue fomu tafadhari.

Simon Kitururu said...

Duh!Mzee naona kimya!Nahisi ni kamsimu fulani hivi kaubize!

MTANZANIA. said...

Da Mija!
Nashukuru sana kwa kunikaribisha katika kinyang'anyiro cha uongozi.Tayari mwanamtandao wetu ameisha jitokeza kuwania moja ya nafasi na tuliobaki tunazidi kuudumisha mtandao hadi hapo uchaguzi utakapoisha. Baada ya hapo mtandao wetu utazikwa rasmi.

Kitururu! Ni kweli nipo kimya na uyahisiyo ndo haswaa yenyewe. Ila chobisi nimekustua kiaina. Vipi ww mtandao wako upo imara kuhakikisha unashinda kwa kishindo tena ka tsunami! Watch up!!!

Simon Kitururu said...

@Duh!Nahitaji kura yako.Labda baada ya hiyo nitashinda:-)

Simon Kitururu said...

Mtanzania eeh!
Nimekumisi, rudi basi AU?

NDABULI said...

Aisee namimi nakuomba urudi ni muda mrefu huonekani Kibarazani kwako.

Simon Kitururu said...

Mtanzania eeeeeeeeeeeeeH!

Kibunango said...

Kamanda Mtz umepotelea wapi?

Anonymous said...

mbona wakuu mmetoka nje ya topic? ha ha ha najua mmepoteana siku nyingi. ebwana urafiki wa hawajamaa na mbwa ni balaa kama hapo ni hadharani ndio mambo kama hayo basi huko ndani nafikiri urafiki unakuwa wa karibu zaidi.. ha ha ah.