Tuesday, January 13, 2009

Mapambano dhidi ya ujinga!!


Mapambano dhidi ya adui ujinga yashika kasi! Shirika la Elimu Kibaha limeanzisha shule ya sekondari maalum kwa wasichana. Shule hii kwa sasa ni ya kutwa na inaitwa "Kibaha Girls' Sec. School. Shule nyingine za sekondari zilizo chini ya Shirika la Elimu Kibaha ni Kibaha Sekondari na Tumbi Sekondari. Vile vile kuna chuo cha maendeleo ya wananchi na chuo cha wauguzi. Karibu Shirika la Elimu Kibaha ujionee!

Karibuni kwa maoni

1 comment:

Simon Kitururu said...

Inatia moyo sana!Mapambano dhidi ya ujinga ni muhimu sana kama nia nikujikwamua.