Tuesday, April 10, 2007

Bifu sasa limekwisha, "sisi wamoja na tuchape kazi".

Pichani "tusameheane mzee kwa yaliyotokea" Kutoka kushoto ni Mh. Spika Sitta , Mh. W/M Lowasa na Mh. Malima. (Picha na Hilary Bujiku)
Siasa bwana ina mambo yake! Mikwara miiiiingi! Binafsi sikuona sababu ya kulumbana sana na kutumia fedha zilizotumika kwa hoja ya Mh. Malima kuhusu muda unaotolewa na ITV kwa viongozi wa kitaifa dhidi ya ule anaopewa Mwenyekiti mtendaji wa IPP katika taarifa za habari za ITV. Hili lilitokea kikao cha bunge kilichopita. Nafikiri kulikuwa na bado kuna hoja nyingine nzito na nyeti zaidi ya hiyo ambazo zilistahili na bado zinastahili mjadala.

3 comments:

Anonymous said...

Hiyo issue ilikuwa ndogo ila ilikuzwa na vyombo vya habari.

mzee wa mshitu said...

Kaka hapa hakuna muafaka wala nini picha hii imetokea kwa bahati mbaya hawa wawili yaani Malima na Lowassa walikuwa wanamsimanga Spika mara na yeye akatokea na wapiga picha waliwataimu tuu. Mambo haya bado kabisa yanachemka.

Mikundu Matako Makalio Manundu said...
This comment has been removed by a blog administrator.