Saturday, January 27, 2007

Nembo za taifa kielelezo cha uzalendo,sheria iruhusu zitumike.


Ama hakika rangi za bendera yetu zinapendeza.
Bendera ni miongoni mwa nembo za taifa na pia ni kitu cha kujivunia kwa kila mwananchi. Kimsingi bendera ni alama ya utaifa na pia ni kielelezo halisi cha uzalendo.Umefika wakati sasa iwe ni ruhusa kwa wananchi kuitumia bendera ya taifa kwani bendera ya taifa ya nchi ndio utambulisho wa nchi na kwa mtu yeyote mzalendo anapoiona bendera ya taifa lake ikipepea mahali fulani, hupata mvuto wa kipekee na pia hukumbuka nyumbani.Mathalani kipindi hiki cha kuinua kandanda Tanzania ni vema ikawa ni ruhusa kwa rangi za bendera kutumiwa na watanzania katika kuishangilia timu ya taifa ya soka na hata timu za taifa za michezo mingine.Vile vile iwe ruhusa kwa watanzania kushona na kununua nguo zenye rangi ya bendera ya taifa tofauti na sasa ambapo watanzania tunabanwa na sheria ya nchi.Mathalani katika mataifa kama Uingereza au Marekani, ni rahisi kukuta nguo, kofia, kalamu, vitambaa na hata makaratasi yenye rangi zinazoonyesha bandera ya nchi hizo yakiwa yamepamba mitaa ya miji. Ni muda muafaka kwa sheria za nchi yetu kufanyiwa marekebisho.Vinginevyo nchi yetu itaendelea kutotambulika na hali kadhalika sifa kemkem za nchi yetu kama vifutio vya utalii vitaendelea kutangazwa kuwa vipo nchini Kenya na wala si Tanzania. Mungu ibariki Tanzania.

1 comment:

Anonymous said...

Kweli flag inapendeza. Hiyo ndo inaitwa "flag chuma, mlingoti chuma".