Monday, January 22, 2007

Wababe wa kivita.

Tukiwa mbele ya sanamu la mashujaa sambamba na "double M" mjini Washington DC.

Katika hali ya kawaida vita si lelemama na wala si suala la kuombea.Ukilinganisha kati ya faida na hasara za vita, haiyumkini hasara zitachukua asilimia kubwa kuliko faida.Pamoja na hayo kuna vita visivyoepukika na vipo vita vya kuepukika.Si lengo langu kujadili aina za vita. Kama picha inavyojieleza, hiyo ni sehemu maalum kwa ajili ya kutunza kumbukumbu ya mashujaa walioshiriki vita vya Vietnam.Nchi ya Marekani inawaenzi kwa namna ya kipekee mashujaa wao al-maarufu kama"wababe wa kivita".Nini somo kwa nchi yetu ambayo miaka ya 1978 ilijikuta katika vita dhidi ya nduli Idd Amin Dada? Binafsi naona umefika wakati sasa kwa serikali ya Tanzania kuwaenzi wapiganaji wetu (wababe wa kivita chini ya amiri jeshi mkuu hayati Mwl. Nyerere) kwa namna walivyojitoa muhanga na hatimaye kuinusuru sehemu ya ardhi ya nchi yetu iliyotaka kuporwa na Nduli. Tuwape heshima stahili wote waliopoteza maisha wakati wa vita na pia washiriki wote ambao bado wapo hai. Mathalani serikali inaweza ikawaenzi kwa kutoa 50% ya ada kwa watoto wa mashujaa walau katika shule za sekondari. Nategemea maoni mujarabu kutoka kwenu.

1 comment:

Anonymous said...

Hata Tanzania huwa tunawakumbuka wababe wa kivita. Kumbuka ile sikukuu ya mashujaa.