Friday, January 26, 2007

Ukitembea utaona au kusikia mengi.

Pichani mwanadada akila pozi na mbwa wake.
Walipata kunena wahenga "ukishangaa ya Musa utayaona ya Firauni". Hawakuishia hapo pia waliibuka na msemo mwingine "tembea uone". Kwa ujumla hizi semi mbili zina maana kubwa iliyofichamana. Mwanamuziki wa kizazi kipya nchini Tanzania ana kibwagizo fulani cha "mbado".Niliwauliza maswali machache marafiki zangu waliopo Tanga na majibu yao yalikuwa mbado. Maswali yangu yalikuwa kama hivi:-
Mimi- Mmewahi kuona mbwa akipigwa busu?
Wao-mbado.
Mimi- Mmewahi kusikia mbwa akiitwa "he" au "she"?
Wao-mbado.
Mimi-mmewahi kusikia mbwa akilala chumba achilia mbali kitanda kimoja na binadamu?
Wao-mbado.
Mimi- jamani hamjayaona wala kuyasikia hayo yote?
Wao-mshangao!!-mbado.
Ndio hivyo hayo mambo yapo.Baada ya kutembea nilibahatika kujua kwamba hayo yote niya kawaida katika jamii za kimagharibi. Mathalani hapa Marekani mbwa hana nafasi kubwa katika suala zima la ulinzi bali ni rafiki mkubwa wa binadamu hali inayopelekea mnyama huyo apewe heshima kubwa na upendo wa hali ya juu. Kupigwa busu, kupewa heshima ya ubinadamu na hata kushea sehemu za kulala ni mambo ya kawaida anayofanyiwa mnyama huyu hapa Marekani. Baada ya kufanya udadisi wa hapa na pale kwa wenyeji wangu wa hapa, majibu niliyopata ni kwamba mnyama mbwa ni rafiki yao mkubwa kwa misingi ya kwamba huwa anawaondolea upweke wale wenye upweke na pia hutoa kampani kwa wasio kuwa na kampani. Bado kwangu imekuwa ngumu kuwaelewa wenzetu hawa na huu urafiki wao kwa hawa wanyama. Uchunguzi wangu usiokuwa rasmi sana unaonyesha wanaume wengi wanakuwa pamoja na mbwa jike na hali kadhalika wanawake wengi wana midume ya mbwa. Nimeiweka hii mada ili nipate maoni kutoka kwa yeyote anayejua lolote juu ya hili suala.

1 comment:

Anonymous said...

Jamaa wanawapenda sana mbwa wao. Ni utamaduni wao kaka sisi hautufai. Poa.