Thursday, February 8, 2007

Heshima nyingine kubwa kwa nchi yetu.

Baadhi ya wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi Tanzania (JWTZ) wanaokwenda kulinda amani nchini Lebanon. Picha na Richard Mwaikenda.

Tanzania imepeleka jumla ya wanajeshi 80 wa Jeshi la Ulinzi Tanzania (JWTZ), kwenda nchini Lebanon kushiriki kulinda amani wakiwa ni sehemu ya vikosi vya Umoja wa Mataifa. Hii pia ni sifa nyingine kwa nchi yetu ikizingatiwa kuwa naibu katibu mkuu wa umoja wa mataifa (UN) pia anatoka Tanzania. Cha msingi ni kwamba askari hao ambao kati yao 11 ni wanawake, kuiwakilisha vyema nchi yetu kwa kuwa na nidhamu na kujiepusha na vitendo vya utovu wa nidhamu kama jeshi linavyoelekeza. Ama hakika hii itakuwa ni nafasi nzuri kuonyesha kwa vitendo yale waliyojifunza na pia kujifunza mengine watakayoyakuta huko kwenye operesheni ya kulinda amani. Mara ya mwisho Tanzania ilitoa askari wake kwenda kulinda amani katika mpango kama huo nchini Liberia kati ya mwaka 1993 na 1995. Mungu ibariki Tanzania na wanajeshi wetu huko Lebanon.

15 comments:

Anonymous said...

Akina mama wa kitanzania huu ni mwaka wao maana wanafanya mambo makubwa!

Simon Kitururu said...

Kweli kabisa nafikiri Tanzania inahitaji kuwepo katika maswala ya kidunia tena.
@Mjeshi-nakubaliana kabisa nauliyosema

MTANZANIA. said...

Ni nafasi nyingine muhimu ya kuitangaza Tanzania kupitia operesheni za kuleta amani duniani.
Lakini idadi hiyo ya wanawake katika msafara huo inatia matumaini kwamba sasa ile kasumba ya kazi hizi za kiume na zile ni za kike yaelekea kufikia tamati.

Unknown said...

kuna jamaa wangu alikuwa kwenye kikosi kilichoenda Liberia.mpaka leo hajalipwa posho waliyoahidiwa.na kwa vile jeshini nidhamu mtondo mmoja,yeye na wenzake hawawezi kuuliziaulizia kuwa seniors!

Anonymous said...

Watu wanaofanya ustadi wa masuala ya unajimu wanasema tunaingia kwenye zama ambazo moja ya alama zake ni nafasi mpya na majukumu mapya wanaopewa wanawake duniani. Wanawake wa India wanalinda amani Liberia. Sasa dada zetu nao hao Lebanoni.

pengine ndio mwanzo wa anguko la mfumo dume.

Anonymous said...

Zemarcopolo,kazi ya jeshi unatakiwa ugangamale na huruhusiwi kudai dai. Jamaa yako asubiri na watamlipa tu.

NDABULI said...

Da Mija sijamsikia kwa hili, da mija kulikoni?

Mija Shija Sayi said...

Ndabuli,
Nia tunayo, uwezo tunao na nguvu tunazo. Ilikuwa ni suala la muda tu, Sasa muda umefika jamii imeanza kutukubali. Lakini pamoja na hayo inabidi tusijisahau safari bado ni ndefu kwetu kina mama hadi kufuta mfumo dume.

Zemarcopolo asante kwa link.

MTANZANIA. said...

Ndesanjo! Yawezekana ndio mwanzo wa mfumo jike huu. Nakumbuka kwamba hata Roma haikujengwa siku moja. Ndabuli na Da Mija naamini kazi kubwa itakuwa ni namna ya kumuwezesha mwanamke hususan wa kijijini maana huko hakuna kabisa nafasi ya mwanamke.
Zemarcopolo! Kasi mpya na ari mpya ilitoa ahadi ya kuboresha maslahi ya wanajeshi ikiwa ni pamoja na kulipa madeni yote ya nyuma. Kwa maana hiyo yawezekana kabisa jamaa yako akalipwa haki yake.

Mija Shija Sayi said...

Mtanzania umeomgea jambo kuhusu mwanamke wa kijijini, lakini si maisha ya mwanamke wa kijijini tu yanayohitaji kukombolea leo hii, mimi naona karibu vitu vyote vijijini vinahitaji kukombolewa. Hebu angali mashule, zahanati, usafiri, halafu angalia vitu kama umeme, maji n.k. Hivi kweli tunavumiliaje kuona wenzetu wakiishi namna ile?

Sijui wenzangu mnasemaje, lakini mimi naona ni wajibu wa kila mmoja wetu kuhakikisha anabadilisha hali ile. Nadhani wakati umefika sasa wa kubeba mabango na kuandamana kwa ajili ya hili.

Zablon Mgonja said...

Inavutia sana namna hii! Safi sana akina dada! Kama wao wanaweza sisi tushindwe kwani tuna nini.... kama wanaume wanaweza, na wanawake nao wanaweza, basi asibakishwe mtu nyuma LAKINI hata kwenye posho, asiachwe mtu nyuma pia. Hili ni jukumu linalohitaji kujitolea haswa kwani lolote laweza tokea, hivyo inapotokea mtu kafanya kazi yake amemaliza, basi apewe chake

Anonymous said...

Tukumbuke kwamba hata Lebanon inayodai kuwa ni nchi secular kuna element kali sana za udini; Waislamu, Mashia(Hizibollah) na Masunni na kati ya Waislamu hao na Wakristo wa Mawârinah/Maronites. Halafu ubaguzi wa makabila kati ya wenyeji Waarabu wenye nchi,Wazungu, Wayahudi, Wakimbizi wa Kipalestina, Waasia, na Waafrika waliopo huko kutafuta maisha .

Tukirejea tukio la Oktoba 1983 ambapo walipuaji mabomu wa kujilipua (kwa mabomu ya kilo zipatazo 5400)waliwalipua na kuwaua zaidi ya askari mia nne wa Kimarekani na takribani askari sitini wa Kifaransa nchini Lebanon! Hoja yangu hapa ni kwamba huyo mwanamama tunayempeleka huko kwa jinsia na rangi yake anaweza kuwa mlengwa wa kivita badala ya mlinzi wa amani.

Mtanzania mwenzenu,

F MtiMkubwa Tungaraza.

Anonymous said...

Tanzanian peacekeepers bombed in Lebanon




MASATO MASATO & AGENCIES
Dar es Salaam

SIX Tanzanian army officers on a peacekeeping mission in Lebanon on Sunday escaped death after being targeted by bombs in the troubled Middle East country.

The Minister for Foreign Affairs and International Cooperation, Mr Bernard Membe, confirmed to THISDAY yesterday that Tanzanian soldiers had just parked their vehicle at a Lebanese checkpoint when a landmine exploded.

Membe said that save for minor damages to the UN four-wheel drive vehicle in which the Tanzanians were travelling, there were no casualties.

’’All our soldiers are fine,’’ he stated.

The attacked soldiers are part of a contingent of 80 military policemen from Tanzania currently on a peacekeeping mission in Lebanon.

It was earlier reported by international media agencies that the blast detonated near the Qasmiyeh bridge on the main coastal road north of Tyre, where the UN Interim Force in Lebanon (UNIFIL) has an observation post.

’’We can confirm that an explosion occurred in the area of Qasmiyeh bridge involving one of our vehicles,’’ UNIFIL deputy spokeswoman Ms Yasmina Bouziane was quoted as saying.

She also affirmed that no casualties had been reported from the incident.

Just last month, a car bomb blast killed six members of UNIFIL’s Spanish battalion in the south of the country. No group claimed responsibility for the June 24 attack but the Spanish government said it suspected it was the work of al Qaeda-inspired Islamist militants.

The UNIFIL has grown to 13,300 troops and naval personnel from 31 countries under a UN security council resolution that halted last year’s conflict between Israel and Lebanese Hezbollah guerrillas.

The UNIFIL troops operate alongside some 15,000 Lebanese soldiers deployed in the south after the July?August war.

Tanzania joined the peace keeping mission in Lebanon last February with the Tanzania People’s Defence Forces (TPDF) sending 80 officers, including 10 women.

Seeing off the officers on February 7, the Chief of Defence Forces, General George Waitara, urged them to adhere to professional soldier ethics while on the international assignment.

Minister Membe said yesterday that the Tanzanian troops were on a six-month assignment in Lebanon which is, however, subject to situational changes.

The six months will elapse next month, but the minister said he was not sure whether the soldiers would be immediately called back or told to stay on.

Unknown said...
This comment has been removed by the author.
Anonymous said...

http://eastafrican.userboard.net/t3-jeshi-la-wananchi-wa-tanzania-jwtz