Kama ni urafiki mhh! "hii too much".

"Wanakumbukwa kwa kuwa walikuja, wakatenda mema na hatimaye wakaondoka". Mimi na wewe tutakumbukwa kwa yapi?. Ni muda muwali sasa kwa mada jadidi kutekelezwa kwa vitendo na si lelemama. Naamini Tanzania yetu itafanikiwa.

Posted by
MTANZANIA.
at
3:16:00 AM
10
comments
Serikali ya Tanzania imedhamiria kuvitangaza vivutio vilivyopo nchini. Hapa ni siku ujumbe wa Tanzania ulipokitembelea chuo kikuu cha New York kwa ajili hiyo. Timu iliongozwa na Mh. Jumanne Maghembe (Waziri wa maliasili na utalii-wa tatu toka shoto). Pia alikuwepo balozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Mh. Mahiga-wa nne toka kulia.
Posted by
MTANZANIA.
at
1:10:00 PM
2
comments
Posted by
MTANZANIA.
at
12:31:00 AM
4
comments
Posted by
MTANZANIA.
at
12:44:00 AM
0
comments
Posted by
MTANZANIA.
at
6:12:00 PM
0
comments

Pichani baba watoto akiwa makini kutoa maelekezo kwa wanawe wanaojaribu kuchora huku mama yao akitazama. Ni njia thabiti ya kuendeleza vipaji.
Posted by
MTANZANIA.
at
7:23:00 PM
3
comments
Pichani "tusameheane mzee kwa yaliyotokea" Kutoka kushoto ni Mh. Spika Sitta , Mh. W/M Lowasa na Mh. Malima. (Picha na Hilary Bujiku)
Posted by
MTANZANIA.
at
6:36:00 PM
3
comments
Moja ya hazina kubwa ya taifa. Anaonekana kama anasema "ok. nipo tayari nipige picha". Pundamilia huyu ni moja ya vivutio vingi vilivyo katika hifadhi ya taifa ya Ngorongoro Crater. Katika karne hii ya sayansi na teknolojia ni muhimu kuvitangaza vivutio hivi. Kama ilivyo habari, biashara pia ni kutangaziana!
Posted by
MTANZANIA.
at
7:46:00 PM
3
comments
Pichani ni makazi ya watu katika mji wa Nashville-TN. Picha nyingi kutoka nchi zilizoendelea huwa ni za kuonyesha mazuri il-hali kutoka Afrika ni za kuonyesha mabaya. Anyway, ninachotaka kukiwakilisha hapa ni kwamba si kila kitu ni shwari katika nchi zilizoendelea kama hii picha ya makazi ya watu katika mji wa Nashville-U.S inavyothibitisha.
Posted by
MTANZANIA.
at
5:17:00 PM
1 comments

Mauaji yaliyotokea nchini Rwanda mwaka 1994 kamwe hayatasahaulika. Si kwa wanyarwanda tu bali hata kwa wapenda amani kote duniani ingawa leo ni miaka 13 tangu yalipotokea. Sababu kubwa ya mauaji ilikuwa ni tofauti za ukabila baina ya makabila makuu mawili yaani wahutu na watutsi. Wengi wa waliouwawa walikuwa ni watutsi na wahutu wachache. Zaidi ya watu 800,000 walipoteza maisha na miongoni mwao 500,000 walikuwa watutsi. (Pia inakadiriwa waliokufa walikuwa zaidi ya 1,000,000). Mauaji haya yalifanywa na vikundi vya wanamgambo wa Kihutu maarufu kama Interahamwe na Impuzamugambi. Zilikuwa takribani siku 100 za umwagikaji wa damu usio na mfano kuanzia April 6 mpaka katikati ya mwezi wa saba. Lakini katika kuadhimisha siku hii hatuna budi kuungana na wenzetu wa Rwanda katika kudumisha udugu,mshikamano na umoja bila kujali tofauti za ukabila,udini na za kisiasa kwani tofauti katika nyanja hizi aghalabu ndio chanzo cha mifarakano miongoni mwa wanajamii. Hongera serikali ya Rwanda kwa mwanzo mzuri wa kuijenga Rwanda mpya yenye uchumi unaokua, miundo mbinu bora na pia huduma bora za kijamii.
Posted by
MTANZANIA.
at
11:14:00 PM
2
comments
Vipaji (talents) mara nyingi huonekana tokea utotoni. Franco akiwa na miaka 7 alifanikiwa kutengeneza gitaa kwa kutumia lililokuwa kopo la bati la kuhifadhia mafuta ya kupikia. Alilitumia gitaa hilo kutoa burudani kwenye mechi za kandanda. Alifanikiwa kupata gitaa halisi alipokuwa na umri wa miaka 11. Wakati huo alikuwa kama mpiga gitaa wa muda tu katika studio ya Loningisa iliyokuwa ikimilikiwa na Wagiriki huko nchini Zaire. Kipindi hicho, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ilikuwa chini ya utawala wa Ubelgiji. Mwaka 1956, Makiadi alifanikiwa rasmi kuanzisha bendi ya OK Jazz ambayo baadaye ilikuja kujulikana kama TPOK Jazz. Aliongeza "TP=Tout Puissant" yenye maana ya "wote wana nguvu". Tizama moja ya kazi zake hapa.
Posted by
MTANZANIA.
at
10:02:00 PM
5
comments
Posted by
MTANZANIA.
at
8:59:00 PM
1 comments
Biashara ya kuuza barafu (ice-cream) ni maarufu sana katika jiji la Dar-es-Salaam. Pichani ni biashara kama hiyo katika jiji la New York. Kwa ujumla mazingira ya biashara hii jijini NY yanafanana kabisa na yale ya jijini Dar-es-Salaam.
Posted by
MTANZANIA.
at
2:54:00 AM
2
comments
Ama hakika Mungu mkubwa! Kutoka kupungua kwa kina cha maji hadi kutapishwa kwa maji katika bwawa la Mtera. Ashukuriwe kwa hilo. Ndio hivyo maji yamejaa pomoni na mamlaka husika imeamua kutapisha maji toka mabwawa ya Mtera na Kidatu. Hakuna atakayesahau uhaba wa umeme uliolikumba taifa mwaka jana. Chanzo cha tatizo kilikuwa ni kupungua kwa maji katika bwawa la Mtera. Leo bwawa limejaa kwa uwezo wake Allah, cha ajabu maji yanatapishwa badala ya kubuniwa njia mbadala za kuyahifadhi kwa ajili ya matumizi ya baadaye endapo yatapungua. Baadhi ya nchi zina utaratibu wa kuhifadhi kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Mathalani Misri ipo Jangwani lakini kwa kutumia maji ya mto Nile wameweza kuhifadhi maji ya kutosha. Kwa maana hiyo hata mto Nile ukikauka hii leo, bado watu wa Misri watakuwa na uhakika wa kupata maji. Tanzania tungeiga mfano wa nchi ya Misri. Kimsingi hakuna sababu ya kumwaga maji yaliyozidi katika mabwawa ya Mtera na Kidatu na badala yake mamlaka husika zingebuni utaratibu wa kuyahifadhi maji hayo kwa ajili ya akiba ili siku zijazo ikitokea yamepungua iwe rahisi kuyatumia pasi kusubiri mvua. Tujifunze kupitia makosa kwani hatuna mkataba na Mungu kwamba mvua itakuwa ya kutosha kila mwaka.
Posted by
MTANZANIA.
at
9:47:00 PM
2
comments
Posted by
MTANZANIA.
at
5:12:00 PM
7
comments
Waziri wa Mali asili na utalii Prof. J4 Maghembe akiteta jambo na wadau wa Chuo kikuu cha New York ikiwa ni jitihada za serikali ya awamu ya nne kuitangaza Tanzania na vivutio mbalimbali vilivyopo nchini. Wadau wa Chuo kikuu cha New York wameonyesha dhamira ya kufungua tawi la chuo hicho nchini Tanzania. Serikali imekipatia chuo hicho ekari 500 kwa ajili ya kufungua tawi hilo ambalo litaitwa NYU in Tanzania. Akiwa chuoni hapo Waziri wa mali asili na utalii aliwahakikishia uwepo wa eneo hilo. Hiyo ilikuwa tarehe 22/2/ 07. Chuo kikuu cha New York tayari kina matawi nchini Brazil, Canada,Uingereza na Ghana. Huenda Tanzania ikaingia kwenye hiyo orodha.
Posted by
MTANZANIA.
at
4:00:00 AM
6
comments
Posted by
MTANZANIA.
at
2:52:00 PM
4
comments
Mh. Waziri mkuu ndugu Edward Lowasa.
Posted by
MTANZANIA.
at
5:02:00 AM
11
comments
Posted by
MTANZANIA.
at
4:28:00 PM
5
comments
"Imepimwa hii na kuthibitishwa na mganga kuwa haina RVF". Nahisi ndivyo asemavyo huyu muuzaji wa duka la nyama jijini Dar es Salaam.
Posted by
MTANZANIA.
at
3:47:00 PM
6
comments
Posted by
MTANZANIA.
at
2:58:00 AM
4
comments
Baadhi ya wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi Tanzania (JWTZ) wanaokwenda kulinda amani nchini Lebanon. Picha na Richard Mwaikenda.
Posted by
MTANZANIA.
at
12:32:00 AM
15
comments
Wachezaji wa timu ya soka ya Taifa (Taifa stars) al-maarufu kama "JK boys" wakiwa mazoezini katika kituo cha mafunzo ya michezo cha Fluminense jijini Rio de Janeiro Brazil. Kutoka shoto ni Mwaikimba, Nsajigwa, Maulid & Yusuf. Picha na Benny Kisaka.
Posted by
MTANZANIA.
at
2:25:00 AM
3
comments
Posted by
MTANZANIA.
at
7:16:00 PM
6
comments
Ni kupumzika tu muda wowote na mahala popote. Picha kutoka darhotwire.
Posted by
MTANZANIA.
at
3:33:00 PM
2
comments
Mh. JK Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akifafanua jambo kuhusu mustakabali wa Taifa letu.
Posted by
MTANZANIA.
at
7:08:00 PM
3
comments
Hali inavyokuwa wakati wa muhadhara katika moja ya kumbi za mihadhara chuo kikuu Mlimani.
Posted by
MTANZANIA.
at
9:01:00 PM
2
comments
(Pichani watanzania waishio Moshi walioamua kutembelea vivutio mbalimbali kama bango linavyojionyesha. Picha kwa hisani ya Juma Iddi Issa -wa kwanza toka kushoto.)
Posted by
MTANZANIA.
at
8:29:00 PM
1 comments
Posted by
MTANZANIA.
at
12:19:00 AM
1 comments
Ama hakika rangi za bendera yetu zinapendeza.
Posted by
MTANZANIA.
at
5:56:00 AM
1 comments
Pichani mwanadada akila pozi na mbwa wake.
Posted by
MTANZANIA.
at
10:40:00 PM
1 comments
(Pichani mwenye batiki ni mke wa mwanaharakati mahiri kutoka Kenya aitwaye Ngugi wa Thiong'o. Wengine ni wanafunzi wa NYU kutoka nchini Tanzania na Kenya.)
Posted by
MTANZANIA.
at
8:09:00 PM
3
comments
Wahenga walinena "kazi na dawa".Ndivyo inavyojidhihirisha katika picha ambapo waafrika mbalimbali waliamua kuifurahia ladha ya taarabu wakati wa sherehe za kuanza muhula wa pili wa masomo hapa NYU. Sipo pichani,ila kabla ya hapo niliwapa shule kidogo namna ya kuicheza na hayo ndo matokeo yake.
Posted by
MTANZANIA.
at
2:00:00 AM
2
comments
Tukiwa mbele ya sanamu la mashujaa sambamba na "double M" mjini Washington DC.
Posted by
MTANZANIA.
at
1:23:00 AM
1 comments
Pichani Mwl. Merchedes Method (katikati) aliye chuo kikuu cha Wisconsin akisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa kocha wa chuo (hayupo pichani) wakati wa mapumziko. Katika mechi hiyo Wisc. walishinda 2-0 huku yeye akiwa kapachika kimiani bao moja.
Posted by
MTANZANIA.
at
2:42:00 AM
2
comments
Muongozo wa dini ya kiislam.
Posted by
MTANZANIA.
at
3:41:00 AM
3
comments
(Pichani Mwl.Ngugi alipolitembelea darasa langu la kiswahili.Umefika wakati kwa serikali ya Tanzania kuwathamini walimu kwani walimu ni funguo za fani anuwai.)
Posted by
MTANZANIA.
at
10:32:00 PM
1 comments
Posted by
MTANZANIA.
at
3:23:00 AM
2
comments